#SAMIA AANZISHA USHIRIKIANO WA KIDICTATOR NA TAORE



 Rais Dictator wa Tanzania Samia Suluhu ameanzisha Uswahiba wa kidictator  (Kiimla) na Rais Dictator Mwenzie
wa Bukina Faso, Captain Ibrahim Taore. Kama wasemavyo waswahili 'Ndege wanaofanana huruka pamoja' Taarifa ambazo hazijawekwa wazi na Serikali ya Tanzania zinazonyesha kuwepo au kuanza kwa ushirikiano kati ya Dar es salaam na Ouagadouggou ambao unasadikiwa kuhusisha Vikosi vya Tanzania katika kusaidia kuiendesha nchi hiyo ya Africa Magharibi ambayo inakabiliwa na athari za kiusalama, magenge au Vikosi hasimu kwa Utawala wa kidictator wa Rais Taore Taarifa zinasema juzi tu ndege iliyowabeba wanajeshi wa Tanzania ilitua kimya kimya usiku wa manane katika uwanja wa kimataifa mjini Ouagadouggou. Hakukuwa shamrashamra zozote au waandishi wa habari kuijuza Dunia kuhusu ziarani hiyo.

Taarifa zilizopatikana awali zinasema kikosi hicho kimekwenda huko kwa ajili ya mafunzo na utafiti wa kijeshi. Hata hivyo Kuna utititi wa maswali kuhusiana na ziara hiyo. Kubwa zaidi ni endapo nchi yenye misukosuko na ukosefu wa kiusalama,inayochechemea kujiimarisha au kujijenga kisiasa , kijamii, au kiuchumi inaweza kuwa uwanja wa mafunzo au utafiti wowote kutoka kwenye nchi iliyotulia kijeshi au kiusalama.

Rais mstaafu wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, alikwenda Burkina Faso katikati ya mwezi Aprili 2025. Ziara yake ilihitimishwa jijini Ouagadougou tarehe 17 Aprili 2025. 

Lengo la Ziara ya Kikwete hata hivo halikufahamika zaidi ya hoja moja tu, kwamba alibena ujumbe Maalum kutoka  kwa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kumkabidhi Kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso, Captain Ibrahim Traoré.

Katika hili ni vema kujitafakari kwamba ni ujumbe gani huu muhimu ambao ungeyarajiwa kutoka Kwa Rais aliyeshinda uchagizi wenye vurugu na utata, kwenda kwa Rais mwingine wa kiimla aliyetwaa madaraka kwa mapinduzi na kisha kuizima demokrasia na kuikalia nchi kimabavu?

Taarifa zilizopatikana baadaye hata hivyo zilisema ziara Ile ililenga kuimarisha uhusiano wa kibalozi, ushirikiano wa kiulinzi, na kubadilishana uzoefu kati ya nchi hizo mbili. Jiulize ni uzoefu upi ambao Tanzania inaweza kupata kutoka Bukina Faso? Hapo ndipo mkakati huu wa siri ulipoanza na mtaalamu huyu wa mikakati, Rais msitaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete 

Ni baada ya Ziara ile ya Kikweye ambapo kikosi Cha jeshi kutoka Tanzania kimepelekwa Bukina Faso. Kulingana na ushirikiano huo, vikosi vya Tanzania vinaenda Burkina Faso kuisaidia nchi hiyo, hasa katika maeneo ya mafunzo na kubadilishana uzoefu wa kiusalama. Hilo huenda linafanyika chini ya kivuli Cha sehemu ya mikakati ya nchi za Afrika kutafuta "suluhisho la Kiafrika kwa matatizo ya Afrika". Lakini ndani ya hoja hizi yapo mambo yaliyofichika.

Nani anatoa mafunzo? Ushirikiano huo unaonekana kuwa wa pande mbili ambapo wataalamu wa Tanzania wanatoa mafunzo na uzoefu katika maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na utawala, ulinzi ,kilimo na madini, huku kubwa zaidi likiwa ushirikiano wa kijeshi.

Sasa nani anamsaidia mwenzake? Huu ni  ushirikiano wa kimkakati. Lakini ni ukweli usiofichika kwamba Tanzania inakwenda kumsaidia Taore kuitawala Bukina Faso. Haya mengine ni kufunika kombe.

Sehemu ya habari hii imetolewa kwenye channel ya Africa perspective miongoni mwa vyanzo vingine.



Post a Comment

Previous Post Next Post