
https://www.blogger.com/blog/post/edit/3207865657537994030/9081263631248039102Kumekuwepo na miito ya mara kadhaa

i) Utekelezaji thabiti wa sheria: Kutoa adhabu kali na za haraka kwa wahalifu ili kuondoa utamaduni wa kutoadhibiwa na kuhakikisha vyombo vya usalama vinachukua hatua za dharura mara tu visa vinaporipotiwa.
ii? Uhamasishaji na elimu: Kuelimisha jamii, hususan wavulana na wanaume, ili kubadili mtazamo na mfumo dume unaochochea chuki na unyanyasaji dhidi ya wanawake.
iii? Vituo vya usaidizi: Kuongeza vituo vya kutoa ushauri nasaha na msaada wa kisaikolojia kwa waathiriwa walio katika hatari.
iv) Uwezeshaji wa kiuchumi: Kuwapa wanawake uhuru wa kifedha ili kuepuka utegemezi unaowafanya wanase katika ndoa au mahusiano yenye ukatili.
v) Kutoa taarifa mapema: Jamii inapaswa kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa za siri kupitia namba za dharura za polisi (kama vile 112 au 999) au kupitia mashirika kama vile UNHCR Kenya.
vi) Elimu na ushauri kwa wanawake na watoto wa kike Kuhusu mahusiano hatari ya kilaghai, kuacha kabisa kulihusisha na hahusiano ya hila na ulaghai wa mapenzi, kuacha kupokea pesa na zawadi kutoka kwa Wanaume ambao wanajua wazi kwamba hawawapendi.
vii) Utoaji wa Elimu na Uhamasishaji kwa vijana kuepuka matumizi ya mihadarati vinavyosababisha kufikiwa maamuzi magumu.
viii) Uwezeshaji wa nafasi za ajira kwa vijana na ushauri nasaha kupunguza msongo wa mawazo kwa vijana.
iX) Serikali itumike vyombo vya habari kuhamasisha Umma, mathalani kama kama ilivyokuwa miaka ya nyuma kwenye Matangazo ya ugonjwa wa Ukimw/HIV/AIDS, kila chombo Cha habari kilirusha Matangazo juu ya ugonjwa huo na mabango yaliwekwa kila sehemu za maeneo ya Umma.
(X) Wazazi na walezi wahimizwe kutoa ushauri nasaha kwa watoto wao, na kuchukua hatua za kinidhamu pale inapobidi, utoaji wa Elimu ya kijamii uanzie katika ngazi ya familia.
Kulingana na mashirika ya kutetea haki za wanawake nchini Kenya, hakuna idadi kamili ya kitaifa iliyotolewa na serikali, lakini ripoti zinaonyesha kuwa zaidi ya wanawake 27 waliuawa kikatili katika kipindi Cha miezi mitatu (3) ya kwanza ya mwaka huu 2026. Hata hivyo, makadirio ya Umoja wa Mataifa huweka wastani wa vifo 47 vya wanawake kila wiki nchini Kenya.
Hapa tumeorodhesha baadhi ya visa vichache kwa kipindi Cha Januari hadi Juni, 2026:
Kisa kilichofungua mwaka 2026 ni Cha Ukatili wa mzazi kwa mtoto kililipotiwa eneo la Dandora, Nairobi,Januari Mosi 2026, Cha mtoto Charlene Nyangweso aliyeadhibiwa kwa kupigwa vibaya na baba yake na kumsababishia kifo, baba yake aliyekuwa ametengana na mama ya mtoto alimwadhibu kwa kosa la kwenda kutembelea mama yake na kuchelewa kurudi.
Visa vinginevyo tulivyoweza kubainishwa taarifa zake ni pamoja na :
#1. Davine Kwamboka (Kaunti ya Migori): Aliuawa kikatili mwezi Aprili, ambapo picha za CCTV zilionyesha mumewe na wanaume wengine wakijaribu kutupa mwili wake.
2. Anita Nyambura (Kaunti ya Nakuru): Aliuawa mwezi Aprili na mumewe ambaye ni mwanajeshi (KDF) mbele ya mtoto wao mchanga.
3. Benedicta Keziah (Kaunti ya Kilifi): Msichana wa umri wa miaka 7 ambaye aliuawa kikatili mnamo mwezi Mei, tukio lililozua hasira kali nchini.
4. Shirley Gatumi (Kaunti ya Tharaka Nithi): Msichana wa miaka mitatu aliyetoweka mnamo Mei na mwili wake kupatikana ukiwa umetenganishwa viungo.
5. Winny: Mwanamke mwenye umri wa miaka 23 aliyepatikana amefariki katika Kijiji cha Kamuga, Nyakach, mnamo Mei 12 baada ya kushambuliwa na mumewe katika mzozo wa nyumbani.
6. Rose Apundi (au Rose Benta Aponia): Mwanafunzi wa miaka 21 wa Riat College ambaye alitoweka Aprili 5, na mwili wake wenye majeraha kupatikana siku chache baadaye ukiwa umetupwa kwenye msitu wa Riat, eneo la Kisumu.
7. Roseline Achieng Odhiambo: Mwanamke wa miaka 37 aliyepatikana Nyumbani mwake, akiwa amefariki na akiwa na majeraha mengi mwilini mwake katika mtaa wa Manyatta 'B' kufuatia shambulio linalohusishwa na unyanyasaji wa nyumbani.
#8. Ann Keya Ahuna aliyeuawa 16 Mei 2026 kwa kuchomwa Kisu na mtu anayesadikiwa kuwa mpenzi wake kwa jina Newton Ambeyi.
9. Sheila -- Kutoka Nyamira Ekerenyo Mwanafunzi mwenye umri miaka 16 aliyeuawa na mtu anayesadikiwa kuwa mpenzi wake ambaye alijinyonga baada kutekeleza kisa hicho.
10. Rachel Wandetto: Mwanamuziki aliyefariki mnamo Mei 19, 2026 baada ya kushambuliwa na kuchomwa moto na watu wasiojulikana.
11. Mercy Nyambura, Mwanafunzi wa Shule ya Msingi ya Sinendet aliyetoweka Mei 18-19,2026 baada ya kutoweka na kupatikana akiwa amekufa kwenye shamba la mahindi.
12.) Abigael Nafula Ogara (32) aliyetoweka Aprili 29,2026 na mwili wake kupatikana kwenye chumba na maiti webuyeMei 22,2026. Inahisiwa kuwa Mwenzi wake askari KDF Bonface Somiyu huenda alihusika na kutoweka kwake, alionekanannaya mara ya mwisho.
13.) Alice Riang'a kutoka Itibo, Suneka Kisii alitoweka Mei 6, 2026, baadaye mwili wake ulipatikana msitu wa Barkowino, Bondo.alizikwa Mei 22, 2026.
14.) Mwanamke kwa jina Jackline Wanjiru (27) alishambuliwa na kumwagiwa Tindikali kwa kile kinachoaminika kama Dhuluma ya kimapenzi, eneo la Kiritili, Embu hatimaye alifariki dunia, Alizikwa Mei 27,2026.
15.) Mwezi wa nne 2026,Mwanamke kwa jina Mercy Awour aliviziwa na kumwagiwa Tindikali na mtu anayesadikiwa kuwa mpenzi wake aliyetumia pikipiki usafiri na kutoweka baada ya tukio hilo.
16. Tarehe 18 Mei, 2026, Mwanamke kwa jina Maurine Masili anauguza majeraha baada ya kudaiwa kumwagiwa maji ya maharage yaliyokuwa yakipikwa jikono baada ya mzozo kuibuka kuhusiana na ubishi juu ya ongezeko la Bei ya Mafuta na msimamo wake kauli ya ''tutam:
17. Mwezi Mei 26, 2026 Mwanafunzi wa kidato Cha nne (17) huko Nakuru anadaiwa kumwagiwa Tindikali na mwanaume 22) anayedaiwa kumlazimisha awe mchumba wake na baada ya kukataliwa alimvizia binti huyo mapema asubuhi akienda Shule na kumwagiwa Tindikali.
18. Mwezi Mei 27, 2026 eneo la Shieni Kaunti ya kirinyaga Mwanaume wa miaka (45) anadaiwa kumuua mpenzi wake mpenzi wake umri miaka (39) baada ya kuibuka mzozo Naina Yao.
19. Tarehe 02 Juni 2026, mwili wa Mwanamke kwa Jina la Salome Chelagat ulipatikana ukiwa uchi kitandani mwake kwenye nyumba ya kupanga eneo la Mucherwo, Molo Kaunti ya Nakuru.
20. Tarehe 11, Juni 2026, Mwili wa Mwanamke kwa Jina Joy Kwanini Gathu ulipatikana kwenye gunia ukiwa umekatwakatwa vipande na kutupwa huko Nyeri. Mwanamke huyo alikuwa na umri wa miaka 25, Muhitimu wa chuo Cha Nyeri Polytechnic.
21. Tarehe 14 Juni, 2026, Mwili wa mwanamke kwa jina Mwanahamisi Juma ulipatikana ukiwa umetupwa kichakani Kijiji Cha Ziwani, eneo la Matuga, kwale kwa kile kinachoaminika alifanyiwa Ukatili kabla ya kuuawa. Mwanamke huyo alikuwa ni bubu.
22..Tarehe 19, Juni 2026, Mwili wa mwanamke kwa jina la Susan Wanjiku Njeri ulitambuliwa na ndugu zake njia alama za vidole na Msimbogeni baada kutoweka kati ya tarehe 11-12, Juni 2026 kutoka eneo la Cieko Kasarani alipokuwa ameanza kazi za ndani (Yaya).
23. Tarehe 23 Juni 2026, mwanamke kwa jina Elizabeth Ngina Mulwa, Umri (2) alikurikana akiwa amekufa, na mwili wake kutenganishwa na kichwa ukiwa uvunguni mwa kitanda kwenye chumba Cha kupanga, eneo la kiang'ombe Thika. Alikuwa Mwanafunzi wa Thika Polytechnic.
24. Tarehe 24 Juni 2026, Mwanaume kwa Jina la Amos Manasseh Nyang'au alishambuliwa na kuuawa na umati wa watu eneo la kerokae, Nyamira, baada ya kusingiziwa kuwa mwizi na mpenzi wake waliokuwa na mgogoro naye. Kijana huyo anadaiwa kwenda kwa mwanamke mpenzi wake kudai mtungi wa gesi alipokuwa ameununua katika mahusiano yao.
25. Tarehe 24, Juni 2026, Msichana mwenye umri wa miaka (17) alishambuliwa Narok na mtu anayemfahamu, na kukatwa mkono na kung'olewa jino (hakufariki ) kwa kile kinachosadikiwa kuwa dhuluma za kingono.
26. Tarehe 30, Juni, 2026, Mwanamke kwa Jina la Teresia Nyokabi alikitikana ameuawa eneo la Gatundu, na mwili wake iliyokuwa uchi ukiwa umetelekezwa.
Hivi ni baadhi ya visa vichache tu lakini uhalisia ni zaidi ya idadi hii.
Toa maoni Yako.....